By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
Tanzania Kids Time
  • Home
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Mazingira
  • Uchambuzi na Takwimu
  • Wasiliana Nasi
Reading: Umuhimu wa Lishe Wakati wa Ujauzito na Unyonyeshaji.
Share
Notification Show More
Latest News
Mapendekezo ya Mradi wa Sauti zetu ni Muhimu kwa Mkakati wa Elimu Jumuishi
Elimu Haki Za Watoto
Mafanikio ya Shirika la SAWA Kuwezesha Wazazi Kuziishi Stadi za Maisha na Maadili
Elimu
Sababu ya Mradi wa ALiVE Kufanikiwa Kutengeneza Vinara Zaidi ya 300 Tanzania
Elimu Haki Za Watoto
KONGANI YA ELIMU YA MTANDAO WA ELIMU WA KIKANDA – RELI AFRIKA YAONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WALIMU DUNIANI.
Elimu
TANZANIA WILL HOST CIGOFA4 TO FIND CONCRETE SOLUTIONS FOR YOUTH LAND QUESTIONS
Editor's Pick
Aa
Aa
Tanzania Kids Time
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Home
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Uchambuzi na Takwimu
  • Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi
  • Contact
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Tanzania Kids Time > Blog > Uncategorized > Umuhimu wa Lishe Wakati wa Ujauzito na Unyonyeshaji.
Uncategorized

Umuhimu wa Lishe Wakati wa Ujauzito na Unyonyeshaji.

Tanzania Kids Time
Last updated: 2024/01/04 at 8:17 AM
By Tanzania Kids Time 4 Min Read
Share
SHARE

 

 Lishe ya wanawake wakati wa ujauzito na kunyonyesha ni muhimu kwa afya ya mama na mtoto aliye tumboni na hata afya ya mtoto mchanga baada ya kuzaliwa. 

Wanawake wanashauriwa kula chakula mchanganyiko na cha kutosha kutoka katika makundi yote ya chakula wakati wa ujauzito na kunyonyesha ili kupunguza athari za kuzaa mtoto mwenye uzito pungufu na matatizo mengine. 

Na wanawake wanaonyonyesha ni muhimu waongeze ulaji wa vyakula vyenye nishati lishe na utomwili kwa wingi zaidi kuliko kiwango kinachoshauriwa kwa wajawazito. 

Hayo yameainishwa na bi, Salome Magembe afisa lishe mkoa wa Morogoro katika semina ilio wakutanisha waandishi wa habari mkoni humo kuhusu kuandika na kuripoti habari zitakazo elimisha jamii kuhusu umuhimu wa unyonyeshaji mtoto maziwa ya mama na lishe kwa mama mjamzito na baada ya kujifungua.

kwa nini kuongeza nishati lishe wakati wa ujauzito?

Aidha mahitaji ya nishati lishe na virutubishi vingine wakati wa ujauzito huongezeka kwa ajili ya kukidhi ongezeko la mahitaji ya mwili wa mama kama vile kuongezeka uzito, kuupa nguvu mwili wakati wa ujauzito na kuweka hifadhi ya nishati lishe ya kutosha itakayotumika wakati wa kunyonyesha. 

Ukuaji wa mtoto aliye tumboni, kondo la nyuma la uzazi na tishu za mfuko wa uzazi, mabadiliko ya utendaji kazi wa moyo na mfumo wa hewa kwa mama

Kuweka uwiano sahihi wa uzito wa mama na kuupa nguvu mwili wakati wote wa ujauzito 

MAHITAJI YA NISHATI LISHE KWA WAJAWAZITO.

Hata hivyo bi, Magembe akazungumzia mahitaji ya nishati lishe na virutubishi vingine mama mwenye ujauzito.

Wanahitaji kula chakula kingi katika kila mlo au kula milo midogo midogo mara kwa mara;

Kula asusa kati ya mlo na mlo;

Kula matunda na mboga mboga kwa wingi katika kila mlo;

Kunywa maji ya kutosha kila siku (glasi 8 au lita 1.5); na

Kuepuka kunywa chai au kahawa pamoja na mlo kwani huzuia ufyonzwaji wa madini ya chuma na huweza kusababisha upungufu wa damu. Ni vyema kunywa chai au kahawa saa moja kabla au baada ya kula.

 Katika hatua nyingine bi,Magembe akazungumzia faida na athari za ongezeko la uzito wakati wa ujauzito. 

Kuongezeka uzito wakati wa ujauzito ni muhimu sana kwani ni kiashiria cha lishe nzuri. Mama anatakiwa kuongezeka wastani wa kilo 12 kwa kipindi chote cha ujauzito. 

Sehemu ya akiba ya mafuta yatatumika kwa ajili ya unyonyeshaji katika miezi michache ya mwanzo 

Ni muhimu kuzingatia kwamba wanawake walio na uzito uliozidi au viribatumbo kabla ya kupata ujauzito hawatakiwi kuongezeka uzito kiwango sawa na wanawake waliokuwa na uzito wa kawaida kabla ya kupata ujauzito. 

Athari za uzito uliozidi wakati wa ujauzito 

Endapo mama atakuwa na uzito uliozidi au kiribatumbo kabla ya ujauzito, au ameongezeka uzito zaidi ya kiwango kinachoshauriwa wakati wa ujauzito anaweza kupata madhara kama vile: 

 

Kisukari cha ujauzito (kiwango kikubwa cha sukari kwenye damu wakati wa ujauzito)

Viashiria vya kifafa cha mimba, hali inayoambatana na shinikizo la juu la damu na kupoteza protini kwenye mkojo.

Matatizo wakati wa kujifungua mfano mtoto kushindwa kutoka kwa njia ya kawaida. 

Matumizi ya vitamini na madini ya nyongeza  

Shirika la Afya Duniani linapendekeza matumizi ya vitamini na madini ya nyongeza hasa madini chuma na asidi ya foliki ili kuzuia upungufu wa wekundu wa damu kwa wanawake wajawazito na wanao nyonyesha, kuzuia kujifungua watoto wenye uzito pungufu, njiti pamoja na kujifungua watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi. 

Nyongeza ya vitamini na madini kwa mjamzito 

You Might Also Like

ENERGY AND NEO-COLONIALISM IN AFRICA, NO ANSWERS?

WAHITIMU WATAKAO JIUNGA DARASA LA KWANZA MWAKA 2023

ATHARI ZA NDOA ZA UTOTONI KIUCHUMI

SIKU YA WATOTO WALIOZALIWA KABLA YA KUKOMAA

ATHARI ZA NDOA ZA UTOTONI KIELIMU

Tanzania Kids Time August 11, 2020
Share this Article
Facebook Twitter Email Print
Previous Article Chanzo cha wiki ya unyonyeshaji 1990 hadi leo.
Next Article Somalia huenda ikahalalisha ndoa za utotoni
Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

Facebook Like
Twitter Follow
Youtube Subscribe
Telegram Follow
- Advertisement -
Ad image

Latest News

Mapendekezo ya Mradi wa Sauti zetu ni Muhimu kwa Mkakati wa Elimu Jumuishi
Elimu Haki Za Watoto
Mafanikio ya Shirika la SAWA Kuwezesha Wazazi Kuziishi Stadi za Maisha na Maadili
Elimu
Sababu ya Mradi wa ALiVE Kufanikiwa Kutengeneza Vinara Zaidi ya 300 Tanzania
Elimu Haki Za Watoto
KONGANI YA ELIMU YA MTANDAO WA ELIMU WA KIKANDA – RELI AFRIKA YAONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WALIMU DUNIANI.
Elimu
//

Tanzania Kids Time: A platform spotlighting children’s and women’s issues in Tanzania, focusing on education, health, and environmental conservation.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

© 2023 Tanzania Kids Time. Powered by Digital Media Innovation Program. All Rights Reserved.

Join Us!

Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..

Zero spam, Unsubscribe at any time.

Removed from reading list

Undo
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?