By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
Tanzania Kids Time
  • Home
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Mazingira
  • Uchambuzi na Takwimu
  • Wasiliana Nasi
Reading: LISHE BORA KWA MTOTO SIKU 1000:
Share
Notification Show More
Latest News
Mapendekezo ya Mradi wa Sauti zetu ni Muhimu kwa Mkakati wa Elimu Jumuishi
Elimu Haki Za Watoto
Mafanikio ya Shirika la SAWA Kuwezesha Wazazi Kuziishi Stadi za Maisha na Maadili
Elimu
Sababu ya Mradi wa ALiVE Kufanikiwa Kutengeneza Vinara Zaidi ya 300 Tanzania
Elimu Haki Za Watoto
KONGANI YA ELIMU YA MTANDAO WA ELIMU WA KIKANDA – RELI AFRIKA YAONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WALIMU DUNIANI.
Elimu
TANZANIA WILL HOST CIGOFA4 TO FIND CONCRETE SOLUTIONS FOR YOUTH LAND QUESTIONS
Editor's Pick
Aa
Aa
Tanzania Kids Time
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Home
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Uchambuzi na Takwimu
  • Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi
  • Contact
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Tanzania Kids Time > Blog > Uncategorized > LISHE BORA KWA MTOTO SIKU 1000:
Uncategorized

LISHE BORA KWA MTOTO SIKU 1000:

Tanzania Kids Time
Last updated: 2024/01/04 at 8:17 AM
By Tanzania Kids Time 8 Min Read
Share
SHARE

Katika mwendelezo wa habari zetu tulizo kwisha zichapisha kupitia tovuti hii kuhusu masuala ya afya ya mama na mtoto hususani Unyonyeshaji maziwa ya mama na lishe kwa mtoto, leo tumekuletea dondoo nyingine kuhusu lishe bora kwa siku 1000 tangu kuzaliwa kwa mtoto,ambapo Afisa Lishe Manispaa ya Morogoro bi,Ester Kawishe anatanabaisha hatua zote muhimu ambazo mzazi/mlezi anapaswa kuzifuata katika kumuhudumia mtoto.

Mtoto anayekuwa na lishe duni katika umri huo ana uwezekano mkubwa wa kudumaa kimwili na kiakili, kuugua mara kwa mara, na hata kufa. 

Madhara ya kilishe yanayojitokeza yasiporekebishwa katika kipindi hiki cha siku 1,000 za mwanzo za maisha ya mtoto huleta athari zisizoweza kurekebishwa tena katika ukuaji na maendeleo yake.

Wizara ya Afya imeainisha vipindi vitatu muhimu vya ulishaji katika maisha ya mtoto. Vipindi hivyo ni:

Miezi 0 – 6

Miezi 6 – 24

Miezi 24 – 59

Aidha bi, Kawishe akazungumzia Ulishaji wa watoto wadogo na wachanga kwa saa ya kwanza hadi miezi 24. 

Saa ya kwanza. 

Mtoto anyonyeshwe maziwa ya mama  ndani ya saa moja baada ya kuzaliwa.

Miezi 6: Mtoto anyonyeshwe maziwa ya mama pekee  kwa miezi sita ya mwanzo.

Miezi 6-24 

Mtoto  aanzishiwe vyakula vya nyongeza atakapotimiza umri wa miezi sita na aendelea kunyonyeshwa  maziwa ya mama mpaka atakapofikisha miaka miwili au zaidi.

Maana ya maneno yanayotumika katika ulishaji wa watoto wachanga na wadogo.

Unyonyeshaji maziwa ya mama pekee 

Tendo la kumpa mtoto maziwa ya mama kwa njia ya kunyonya kutoka kwenye titi, au kupewa maziwa ya mama yaliyokamuliwa kwa kutumia kikombe, bila kumpa vinywaji au vyakula vingine ikiwemo maji, isipokuwa dawa na chanjo kwa ushauri wa mtaalamu wa afya. 

Ulishaji watoto vyakula vya nyongeza 

Mchakato wa kuanza kumpa mtoto vyakula vya nyongeza atakapofikisha umri wa miezi 6 kwa kuwa maziwa ya mama pekee hayatoshelezi mahitaji yake ya kilishe. Mtoto apewe vinywaji na vyakula vingine huku akiendelea kunyonyeshwa.

Hata hivyo bi, Kawishe  aka fafanua Taratibu za Unyonyeshaji.

Maziwa ya mama ni chakula cha kipekee – hakiwezi kuigwa. 

Kina uwiano sahihi wa virutubishi, kimetengenezwa kwa usahihi kutumiwa na mtoto wa binadamu na hubadilika kulingana na mabadiliko ya mahitaji ya mtoto kulingana na umri. 

Ingawa kunyonyesha ni tendo la kiasili, mama anahitaji kujifunza mbinu na kanuni za kunyonyesha vizuri.

Mwili wa mama ugusane na mwili wa mtoto ngozi kwa ngozi mara tu baada ya kujifungua.

Mtoto anyonyeshwe ndani ya saa moja baada ya kujifungua. 

Kunyonyesha maziwa ya mama pekee kuanzia mtoto anapozaliwa hadi anapotimiza umri wa miezi 6.

Kunyonyesha mtoto mara kwa mara wakati wote usiku na mchana 

Kuyonyesha mtoto kila wakati kadiri anavyohitaji.

Mtoto anyonye na kumaliza maziwa yote kwenye titi moja na aachie mwenyewe kabla ya kumhamishia kwenye titi lingine.

Mpakate na kumweka mtoto vizuri kwenye titi.

Faida za Unyonyeshaji.

Kupungua kwa uwezekano wa kupata tatizo la manjano 

Kuboresha ukuaji na hali ya lishe ya mtoto 

Kupungua kwa vifo vrisha kingamwili ya mtoto 

kupungua kwa maambukizi 

Kupungua kwa magonjwa ya ngozi 

kupungua kwa magonjwa ya mfumo wa njia ya chakula 

Kupungua kwa magonjwa ya kuharisha 

Kupungua kwa magonjwa ya mfumo wa njia ya hewa 

Kuboresha mahusiano baina ya mama na mtoto 

Kupungua kwa uwezekano wa magonjwa sugu (kisukari, magonjwa ya moyo, pumu na baadhi ya saratani)

Kupunguza uwezekano wa kuwa na uzito uliozidi au kiribatumbo 

Kuboresha ukuaji wa kiakili na misuli.

Faida kwa mama 

Kupunguza upotevu wa damu baada ya kujifungua 

Kupunguza sononi (depression) baada ya kujifungua 

Kupunguza uwezekano wa kupata ujauzito mapema katika miezi sita ya mwanzo endapo mama atanyonyesha maziwa ya mama pekee 

Kupunguza uwezekano wa kupata baadhi ya saratani kama: 

Saratani ya via vya uzazi mfano Shingo ya uzazi 

Saratani ya matiti 

Mama kurudia hali yake ya kawaida mapema kimaumbile na kupunguza uzito uliotokana na ujauzito.

MADHARA YA ULISHAJI MBADALA KWA WATOTO.

Athari kwa mtoto ni: 

Ukuaji duni na utapiamlo 

Kuongezeka kwa vifo 

Kuongezeka kwa magonjwa mbalimbali:

Maambukizi kwenye masikio 

Magonjwa ya ngozi 

Magonjwa ya mfumo wa njia ya chakula 

Kuhara 

magonjwa ya njia ya mfumo wa hewa 

Kuathiri mahusiano ya mama na mtoto 

Uwezekano mkubwa wa magonjwa sugu (kisukari, magonjwa ya moyo na baadhi ya saratani)

Kuongezeka kwa uwezekano wa kuwa na uzito uliozidi na kiribatumbo 

Kupata alama za chini (IQ) kwenye mitihani ya majaribio ya ufahamu kiakili.

Athari za kutonyonyesha mtoto.

Athari kwa mama 

Sonona au msongo wa mawazo baada ya kujifungua 

Uwezekano wa kupata ujauzito mwingine mapema 

kuongezeka kwa uwezekano wa kupata baadhi ya saratani kama:

Saratani ya via vya uzazi 

Saratani ya matiti 

Kuchelewa kupunguza uzito uliotokana na ujauzito na hivyo kushindwa kurudia hali yake ya kawaida mapema baada ya kujifungua.

Kukabiliana na Imani Potofu na Changamoto za Unyonyeshaji.

Baadhi ya imani potofu na changamoto za unyonyeshaji ni pamoja na: 

Maziwa ya mama hayatoshi katika siku tatu za mwanzo baada ya kujifungua, na hata kidogo yanayotoka hayafai kumpa mtoto, inafaa kumpa mtoto asali, maji yenye sukari, au maziwa mbadala katika kipindi hiki.”

ii. “Wingi wa maziwa ya mama unategemea chakula na tabia za ulaji za mama, pia vyakula vingi huathiri afya ya mtoto. Kama mama anakula vyakula vya moto mtoto atapata tatizo la kuhara na kama mama atakula vyakula vya baridi, mtoto atapata tatizo la kukohoa.”

iii. “Wakati anaponyonyeshwa, mtoto anahitaji maji ya nyongeza hususani hali ya hewa inapokuwa ya joto.”

iv. “Kama mama ana matiti madogo, atatengeneza kiasi kidogo cha maziwa.”

v. “Kama mama amejifungua kwa njia ya upasuaji hatakiwi kumnyonyesha mtoto.”

vi. “Mtoto anayeharisha asinyonyeshwe maziwa ya mama.”

“Mtoto mwenye umri wa miezi 3 anaweza kuachishwa kunyonya na kuanzishiwa vyakula mbadala ili mama yake arudi kazini.”

ULISHAJI WATOTO VYAKULA VYA NYONGEZA.

Katika hatua nyingine afisa lishe akasema nibora kufuata taratibu zinazo shauriwa na wataalamu wa afya na Shirika la Afya Duniani linavyopendekeza: 

“kuwaanzishia watoto vyakula vya nyongeza katika umri muafaka wa miezi 6 huku akiendelea kunyonyeshwa maziwa ya mama mpaka atakapofikisha umri wa miaka miwili au zaidi.” 

Inapendekezwa kumwanzishia mtoto vyakula vya nyongeza anapotimiza umri wa miezi 6 kwa sababu : 

Mahitaji yake ya nishati lishe na virutubishi yameongezeka na maziwa ya mama pekee hayawezi kutosheleza mahitaji hayo.

Kuanzisha ulishaji wa vyakula vya nyongeza kabla ya umri wa miezi 6 kunaweza kusababisha kuongezeka kwa uwezekano wa mtoto kupata maambukizi hususani kuhara.

Kiumri wanakuwa tayari na uwezo wa kula vyakula vingine.

Itaendelea ……….

You Might Also Like

ENERGY AND NEO-COLONIALISM IN AFRICA, NO ANSWERS?

WAHITIMU WATAKAO JIUNGA DARASA LA KWANZA MWAKA 2023

ATHARI ZA NDOA ZA UTOTONI KIUCHUMI

SIKU YA WATOTO WALIOZALIWA KABLA YA KUKOMAA

ATHARI ZA NDOA ZA UTOTONI KIELIMU

Tanzania Kids Time August 12, 2020
Share this Article
Facebook Twitter Email Print
Previous Article Somalia huenda ikahalalisha ndoa za utotoni
Next Article Lishe endelevu kwa maendeleo ya taifa
Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

Facebook Like
Twitter Follow
Youtube Subscribe
Telegram Follow
- Advertisement -
Ad image

Latest News

Mapendekezo ya Mradi wa Sauti zetu ni Muhimu kwa Mkakati wa Elimu Jumuishi
Elimu Haki Za Watoto
Mafanikio ya Shirika la SAWA Kuwezesha Wazazi Kuziishi Stadi za Maisha na Maadili
Elimu
Sababu ya Mradi wa ALiVE Kufanikiwa Kutengeneza Vinara Zaidi ya 300 Tanzania
Elimu Haki Za Watoto
KONGANI YA ELIMU YA MTANDAO WA ELIMU WA KIKANDA – RELI AFRIKA YAONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WALIMU DUNIANI.
Elimu
//

Tanzania Kids Time: A platform spotlighting children’s and women’s issues in Tanzania, focusing on education, health, and environmental conservation.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

© 2023 Tanzania Kids Time. Powered by Digital Media Innovation Program. All Rights Reserved.

Join Us!

Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..

Zero spam, Unsubscribe at any time.

Removed from reading list

Undo
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?