By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
Tanzania Kids Time
  • Home
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Mazingira
  • Uchambuzi na Takwimu
  • Wasiliana Nasi
Reading: MIMBA ZA UTOTONI ZIMEONGEZEKA MKOA WA MOROGORO KUTOKA 800 HADI ZAIDI YA 1200
Share
Notification Show More
Latest News
Mapendekezo ya Mradi wa Sauti zetu ni Muhimu kwa Mkakati wa Elimu Jumuishi
Elimu Haki Za Watoto
Mafanikio ya Shirika la SAWA Kuwezesha Wazazi Kuziishi Stadi za Maisha na Maadili
Elimu
Sababu ya Mradi wa ALiVE Kufanikiwa Kutengeneza Vinara Zaidi ya 300 Tanzania
Elimu Haki Za Watoto
KONGANI YA ELIMU YA MTANDAO WA ELIMU WA KIKANDA – RELI AFRIKA YAONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WALIMU DUNIANI.
Elimu
TANZANIA WILL HOST CIGOFA4 TO FIND CONCRETE SOLUTIONS FOR YOUTH LAND QUESTIONS
Editor's Pick
Aa
Aa
Tanzania Kids Time
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Home
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Uchambuzi na Takwimu
  • Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi
  • Contact
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Tanzania Kids Time > Blog > Afya > MIMBA ZA UTOTONI ZIMEONGEZEKA MKOA WA MOROGORO KUTOKA 800 HADI ZAIDI YA 1200
AfyaUchambuzi na Takwimu

MIMBA ZA UTOTONI ZIMEONGEZEKA MKOA WA MOROGORO KUTOKA 800 HADI ZAIDI YA 1200

Tanzania Kids Time
Last updated: 2024/01/29 at 2:30 PM
By Tanzania Kids Time 3 Min Read
Share
SHARE

 

   Pichani ni Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Morogoro Bi, Jissica Kagunila

Matukio ya Mimba za utotoni yaliyoripotiwa Ofisi ya
Afisa ustawi wa Jamii Mkoa wa Morogoro, yaliongezeka kutoka 800 mwaka 2019/2020
hadi kufikia zaidi ya 1200 Mwaka 2020/2021.

Akithibitisha Takwimu hizo Afisa usatawi wa Jamii Mkoa
wa Morogoro Bi, Jessica Kagunila, alisema sababu ya Mimba za utotoni kuongezeka
inachangiwa na Mila na Desturi za Mkoa huo pamoja na malezi yasiyo mazuri ya
watoto.

“Tukianza
kwa Mwaka 2019/2020 matukio ya mimba za utotoni yaliyoripotiwa ni 800 lakini
tukija kwa Mwaka 2020/2021 yameongezeka hadi kufikia zaidi ya 120, hii ni
kutokana na Mila na desturi na malezi yasiyo mazuri kwa upande wa walezi na
wazazi’’ alisema Jessica Kagunila

Kwa mujibu wa Ofisi ya muendesha Mashtaka Mkoa wa
Morogoro DPP, matukio ya mimba za utotoni ambayo kisheria huitwa matukio ya
ubakaji yanaongezeka kutokana na watuhumiwa wa makossa hayo kutoa Rushwa kwa
waathirika na kesi kukosa ushahidi Mahakamani, alisema kaimu uendesha mashtaka
wa Mkoa wa Morogoro Flora Massawe.

“Inatokea
mara nyingi mahakamani, mashahidi wengi ambao ni wahanga watoto wanakuja
kugeuka yaani ule ushahidi waliotoa Polisi kwamba wamefanyiwa kitendoi cha
ubakaji na flani wakifika mahakamani wanakuja kukataa, na hii tumebaini
kutokana na wazazi kuridhia kufanya makubaliano na mtuhumiwa kuna kiasi cha
Pesa wanalipana, basi huku kesi zinaharibika’’ alisema Flora Massawe

Afisa ustawi wa Mkoa wa Morogoro Bi, Jessica alieleza
namna ambavyo watazidi kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha matukio
ya Mimba na Ndoa za utotoni yanapungua.

Bi,
Jessica alisema
“Elimu sio suala la ustawi wa Jamii peke
yake, maendeleo ya Jamii na wadau wengine wa Elimu tutaendelea kushirikiana kuzunguka
shuleni kutoa elimu na hata kuwafikia wazazi kadri tutakavyoweza pamoja na
walimu ambao wanakaa muda mrefu na watoto’’

Katika kumulikia juhudi za Sekta binafsi kushirikiana
na Serikali juu ya kutokomeza Mimba za utotoni Mkoa wa Morogoro, Tanzania kids
time ilizungumza na Mratibu wa Miradi Evarist Momburi, kutoka Shirika la SAWA
WANAWAKE TAZNANIA lililojikita katika kusimamia ulizi wa Mtoto na utoaji Elimu
jumuishi kwa Shule za Msingi, ili kusikia maoni yake pamoja na juhudi zao
katika hili.

“kama
tunataka tupunguze hili tatizo la Mimba za utotoni, dawa yake ni kujenga mabweni
na kujenga Shule shikizi ambazo zitasaidia kupunguza ule umbali wa mwanafunzi
kutembea kuifata Shule ilipo, na hili tulifanya utafiti tukagundua watoto wengi
walikuwa wanakatiza masomo kwa sababu walikua wanapata changamoto ya umbali kuifata Shule ilipo’’

Alisema katika Mkoa wa Morogoro Shirika la, SAWA
WANAWAKE TANZANIA tayari limeshaboresha mabweni ya wasichana katika Shule za
Sekondari za DOMA na MVOMERO na Mwaka 2022 wamejipanga kuifikia Shule ya
Sekondari WAMI DAKAWA kupitia Mradi wake wa TUWALINDE WATOTO.

 

 

 

You Might Also Like

THROUGH MZF NOW TRADITIONAL BIRTH ATTENDANCE THEY IMPROVE WOMEN’S WELL-BEING FOR SAFE DELIVERY

TOWARDS TEN YEARS OF MILELE ZANZIBAR FOUNDATION, READ THE ACHIEVEMENTS OF THE SHEHIA PROJECT

MABADILIKO YA HALI YA HEWA NITISHIO LINALOWAKABILI WANAWAKE WAJAWAZITO NA WATOTO.

MTI WA MATUMAINI WA ZINDULIWA ARUSHA: UNICEF

LISHE BORA NI MTAJI: NIMUHIMU KUWEKEZA KWA WATOTO,FAO:

Tanzania Kids Time February 15, 2022
Share this Article
Facebook Twitter Email Print
Previous Article MAHAKAMA YAWAFIKIA WANANCHI ZAIDI YA 30,000 KUWAPA ELIMU YA SHERIA NDANI YA SIKU 7, MOROGORO
Next Article WANAFUNZI NA WALIMU WAELEZEA MANUFAA, KUKAMILIKA MRADI WA MADARASA YA UVIKO19
Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

Facebook Like
Twitter Follow
Youtube Subscribe
Telegram Follow
- Advertisement -
Ad image

Latest News

Mapendekezo ya Mradi wa Sauti zetu ni Muhimu kwa Mkakati wa Elimu Jumuishi
Elimu Haki Za Watoto
Mafanikio ya Shirika la SAWA Kuwezesha Wazazi Kuziishi Stadi za Maisha na Maadili
Elimu
Sababu ya Mradi wa ALiVE Kufanikiwa Kutengeneza Vinara Zaidi ya 300 Tanzania
Elimu Haki Za Watoto
KONGANI YA ELIMU YA MTANDAO WA ELIMU WA KIKANDA – RELI AFRIKA YAONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WALIMU DUNIANI.
Elimu
//

Tanzania Kids Time: A platform spotlighting children’s and women’s issues in Tanzania, focusing on education, health, and environmental conservation.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

© 2023 Tanzania Kids Time. Powered by Digital Media Innovation Program. All Rights Reserved.

Join Us!

Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..

Zero spam, Unsubscribe at any time.

Removed from reading list

Undo
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?