By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
Tanzania Kids Time
  • Home
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Mazingira
  • Uchambuzi na Takwimu
  • Wasiliana Nasi
Reading: VIJANA WAOMBA SOMO LA STADI ZA MAISHA KUFUNDISHWA SHULENI
Share
Notification Show More
Latest News
Mapendekezo ya Mradi wa Sauti zetu ni Muhimu kwa Mkakati wa Elimu Jumuishi
Elimu Haki Za Watoto
Mafanikio ya Shirika la SAWA Kuwezesha Wazazi Kuziishi Stadi za Maisha na Maadili
Elimu
Sababu ya Mradi wa ALiVE Kufanikiwa Kutengeneza Vinara Zaidi ya 300 Tanzania
Elimu Haki Za Watoto
KONGANI YA ELIMU YA MTANDAO WA ELIMU WA KIKANDA – RELI AFRIKA YAONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WALIMU DUNIANI.
Elimu
TANZANIA WILL HOST CIGOFA4 TO FIND CONCRETE SOLUTIONS FOR YOUTH LAND QUESTIONS
Editor's Pick
Aa
Aa
Tanzania Kids Time
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Home
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Uchambuzi na Takwimu
  • Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi
  • Contact
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Tanzania Kids Time > Blog > Elimu > VIJANA WAOMBA SOMO LA STADI ZA MAISHA KUFUNDISHWA SHULENI
ElimuUncategorized

VIJANA WAOMBA SOMO LA STADI ZA MAISHA KUFUNDISHWA SHULENI

Tanzania Kids Time
Last updated: 2024/01/29 at 2:30 PM
By Tanzania Kids Time 4 Min Read
Share
SHARE

Katika juhudi za kuendelea kuunga Mkono lengo la namba Nne la umoja wa mataifa la kuboresha Elimu bora, nchini Tanzania baadhi ya vijana wameeleza kukosa maarifa ya Stadi za maisha ambayo wangeweza kufundishwa katika mtaala wa Elimu iwasaidie kujitambua na kupanua fikra zao, maarifa na kuwa wabunifu hata baada ya kuhitimu masomo.


Chini ya shirika la Milele Zanzibar Foundation na Uwezo Tanzania, tathmini ya upimaji stadi za maisha kwa vijana wa umri wa miaka 13 hadi 17 inaendelea kufanyika Tanzania Bara katika awamu ya pili huku ambapo upande wa Jiji la Dar es salaam vijana wameendelea kufanyiwa tathmini katika Halmashauri za Wilaya ya Ilala na Kinondoni.

Kwa mujibu Ripoti ya mustakabali wa kazi iliyotolewa na Foramu ya kiuchumi ya Dunia Oktoba 2020 inaonesha ukosefu wa stadi za maisha unazidi kuwa mkubwa katika Ajira, na hadi kufikia Mwaka 2025 45% ya waajiri watahitaji waajiriwa wenye maadili ya stadi za maisha badala ya kuwajengea uwezo na mafunzi wakishaajiriwa hii ni kutokana na mfumo wa Elimu jinsi unavyowaandaa wahitimu kuwa tegemezi.

Elizabeth Lazaro ni msichana anayesoma kidato cha Nne Shule ya Sekondari BUYUNI Kata ya PUGU katika Jiji la ILALA, baada ya kufanyiwa utafiti akiulizwa maswali alisema ni dhahili kuna umuhimu wa Serikali kuongeza Somo la Stadi za Maisha katika mtaala wa Elimu ili kukisaidia kizazi chao kuwa na maarifa zaidi ya Elimu ya kawaida yatakayo wasaidia kujitegemea na kuwa msaada kwa Jamii.

“Katika maswali haya niliyoulizwa nimejifunza mengi, nimejifunza jinsi ya kumtetea mtu, nashukuru kwa uelewa huu unatusaidia, kwa sababu katika Jamii vijana wanachukuliwa kama ni watu wasio faa, kama wanatabia mbaya, ikiingia mashuleni itasaidia sana kwa sisi vijana kujitambua’’ alisema Elizabeth

Athumani Kihagila kutoka Kata ya PUGU Jiji la ILALA ni mmoja wa watafiti wanaododosa vijana, alisema uzoefu alioupata kote alikopita kuhoji, vijana wengi walikosa maarifa ya ziada katika kujibu maswali huku akigusia suala la wanafunzi kushindwa kutumia vifaa vya kidigitali katika ujifunzaji.

Athumani alisema ‘’kwa tathmini niliyoifanya kwa vijana, kwanza wengi kusoma kwa kutumia vifaa vya kidijitali wengi uwezo wao uko chini wachache sana wanaweza, kama Serikali ingeweza kuweka somo la stadi za maisha kama yalivyo masomo mengine Shuleni, ingesaidia sana kwani ni jambo ambalo linahitajika sana’’

Mratibu wa mradi wa ALiVE Halmashauri ya Wilaya ya Kinondoni, TUNU SANGA alisema watatumia matokeo ya tathmini ya stadi za maisha kwa vijana kushirikiana na Serikali kuboresha mitaala ili kuwasaidia vijana kulitumikia vyema Taifa lao.

‘’Zoezi hili litatuwezesha kuweza kushirikiana na Serikali kuja na mbinu mbadala za kuweza kuboresha namna gani vijana wa kitanzania wanaweza kupata Elimu ya stadi za maisha ili tuondokane na dhana za kusema vijana hawajitambui’’ alisema Tunu sana
Ripoti ya hali ya maadili ya stadi za maisha kwa vijana Tanzania na Afrika mashariki inatarajiwa kutoka Mwezi wa Tisa 2022, ambayo inalenga kuleta ushawishi wa mabadiliko ya Sera na mitaala ya Elimu kujumuisha Somo la stadi za maisha shuleni.
Na. Hamad Rashid.

You Might Also Like

Mapendekezo ya Mradi wa Sauti zetu ni Muhimu kwa Mkakati wa Elimu Jumuishi

Mafanikio ya Shirika la SAWA Kuwezesha Wazazi Kuziishi Stadi za Maisha na Maadili

Sababu ya Mradi wa ALiVE Kufanikiwa Kutengeneza Vinara Zaidi ya 300 Tanzania

KONGANI YA ELIMU YA MTANDAO WA ELIMU WA KIKANDA – RELI AFRIKA YAONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WALIMU DUNIANI.

ENERGY AND NEO-COLONIALISM IN AFRICA, NO ANSWERS?

Tanzania Kids Time August 11, 2022
Share this Article
Facebook Twitter Email Print
Previous Article KUWA NA MAAMBUKIZI YA VVU SIO SABABU YA KUTOKUWA NA MPENZI.
Next Article WANAWAKE WANAONYONYESHA WAAHIDI KUZINGATIA MLO WA MAKUNDI MATANO YA VYAKULA
Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

Facebook Like
Twitter Follow
Youtube Subscribe
Telegram Follow
- Advertisement -
Ad image

Latest News

Mapendekezo ya Mradi wa Sauti zetu ni Muhimu kwa Mkakati wa Elimu Jumuishi
Elimu Haki Za Watoto
Mafanikio ya Shirika la SAWA Kuwezesha Wazazi Kuziishi Stadi za Maisha na Maadili
Elimu
Sababu ya Mradi wa ALiVE Kufanikiwa Kutengeneza Vinara Zaidi ya 300 Tanzania
Elimu Haki Za Watoto
KONGANI YA ELIMU YA MTANDAO WA ELIMU WA KIKANDA – RELI AFRIKA YAONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WALIMU DUNIANI.
Elimu
//

Tanzania Kids Time: A platform spotlighting children’s and women’s issues in Tanzania, focusing on education, health, and environmental conservation.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

© 2023 Tanzania Kids Time. Powered by Digital Media Innovation Program. All Rights Reserved.

Join Us!

Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..

Zero spam, Unsubscribe at any time.

Removed from reading list

Undo
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?