By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
Tanzania Kids Time
  • Home
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Mazingira
  • Uchambuzi na Takwimu
  • Wasiliana Nasi
Reading: WANAWAKE WANAONYONYESHA WAAHIDI KUZINGATIA MLO WA MAKUNDI MATANO YA VYAKULA
Share
Notification Show More
Latest News
Mapendekezo ya Mradi wa Sauti zetu ni Muhimu kwa Mkakati wa Elimu Jumuishi
Elimu Haki Za Watoto
Mafanikio ya Shirika la SAWA Kuwezesha Wazazi Kuziishi Stadi za Maisha na Maadili
Elimu
Sababu ya Mradi wa ALiVE Kufanikiwa Kutengeneza Vinara Zaidi ya 300 Tanzania
Elimu Haki Za Watoto
KONGANI YA ELIMU YA MTANDAO WA ELIMU WA KIKANDA – RELI AFRIKA YAONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WALIMU DUNIANI.
Elimu
TANZANIA WILL HOST CIGOFA4 TO FIND CONCRETE SOLUTIONS FOR YOUTH LAND QUESTIONS
Editor's Pick
Aa
Aa
Tanzania Kids Time
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Home
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Uchambuzi na Takwimu
  • Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi
  • Contact
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Tanzania Kids Time > Blog > Afya > WANAWAKE WANAONYONYESHA WAAHIDI KUZINGATIA MLO WA MAKUNDI MATANO YA VYAKULA
AfyaUncategorized

WANAWAKE WANAONYONYESHA WAAHIDI KUZINGATIA MLO WA MAKUNDI MATANO YA VYAKULA

Tanzania Kids Time
Last updated: 2024/01/29 at 2:30 PM
By Tanzania Kids Time 3 Min Read
Share
SHARE

Wanawake wanaonyonyesha watoto, wameahidi kuzingatia mlo wa makundi matano ya Chakula ili kujenga na kulinda Afya ya Mtoto aliye chini ya umri wa miaka Sita, katika ukuaji wa akili na Mwili wake.


Hamad Rashid, alihudhuria sherehe za maadhimisho ya Wiki ya unyonyeshaji Mkoa wa Morogoro yaliyofanyika katika viwanja vya Kata ya Mkambalani Kijiji cha Mkambalani Manispaa ya Morogoro na kuandaa Makala ifuatayo.

Fadhila Yusufu ni mmoja wa wanawake waliohudhuria maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji mtoto maziwa ya mama na ana mtoto mwenye umri wa miezi sita. Mama huyu ni mkazi wa kijiji cha Mkambalani, hapo hapo mkoani Morogoro, alisema unyonyeshaji kwake ndio kipaumbele kikubwa kwa mtoto wake.

“sasa hivi tulivyotoka hapa inamaana tutaongeza juhudi za unyonyeshaji kwanza Dakika 45 mpaka dakika 60.” Na mimi uji lishe huwa natengeneza mwenyewe ukiwa na makundi manne ya chakula halafu Tunda kama kundi la Tano natumia baada ya kumalisha kupika uji’’ alisema Fadhila Yusufu
Mtoa huduma za afya kitengo cha Mama na Mtoto katika Zahanati ya Kata ya Mkambalani Rebeka Wami alithibitisha wanawake kuwa na mwamko wa kunyonyesha watoto wao kwa mujibu wa malekezo ya wataalamu wa afya.

“Katika siku yetu hii ya unyonyeshaji, tumeweza kupata uzoefu wa kipekee ambao tumeona akina mama wengi wanahamasika na unyonyeshaji wa maziwa pekee kwa mtoto chini ya miezi sita. Na ukanda huu akina mama wengi wanaonekana wamepata elimu na elimu hii imeweza kuwasaidia kunyonyesha watoto wao na kuondoa hali ya utapiamlo.” Alieleza mtoa huduma ya afya, Rebeka Wami.

RAJABU SHABANI Baba wa Familia katika Kijiji cha Mkambalani alisema katika kipindi cha mke wake kunyonyesha huwa anawajibika ipasavyo kumhamasiha.Rajabu alisema,

“mimi huwa namsaidia kazi mke wangu akiwa ananyonyesha labda naosha vyombo au kufua yeye akiwa anamnyonyesha Mtoto n ahata yeye akiwa anakazi nambeba Mtoto, nawahamasisha akina Baba wengine kuwasaidia wake zao shughuli ndogo ndoto pindi wanaponyonyesha”

Akizungumzia malengo ya wiki ya unyonyeshaji Afisa Lishe Manispaa ya Morogoro Bi ESTHER CHACHA alieleza pia kwamba “Mtoto anaponyonya maziwa ya Mama kwa muda wa miezi sita bila kula na kunywa chochote inamsaidia katika kukua akiwa na akili nzuri, kumpa kinga ya asilia ya Mwili na niwaambie maziwa ya Mama yanakila aina ya virutubisho anavyopashwa kupewa Mtoto”
Bi, Esther aliongeza kuwa “ni muhimu sana Mtoto kunyonyeshwa ndani ya saa moja baada ya kuzaliwa kwani yale maziwa huwa ndio yanakinga nyingi kwa Mtoto na husaidia kukata Damu kwa Mama aliyejifunua”

Sherehe za maadhimisho ya Wiki ya Unyonyeshaji kimkoa zimeandaliwa Serikali la Mkoa wa Morogoro kwa kushirikiana na Shirika la save the children kupitia mradi wake wa USAID LISHE ENDELEVU kwa hisani ya watu wa Marekani.

Aidha chanjo ya Vitamin A na dawa za minyoo zilitolewa kwa watoto wa miezi sita hadi miaka mitano katika maadhimisho hayo ilihali burudani ya muziki wa mwambao umetolewa na Mtumbuizaji MARIAM MAMBO kupambiza sherehe hizo.

Na Hamad Rashid.

You Might Also Like

ENERGY AND NEO-COLONIALISM IN AFRICA, NO ANSWERS?

THROUGH MZF NOW TRADITIONAL BIRTH ATTENDANCE THEY IMPROVE WOMEN’S WELL-BEING FOR SAFE DELIVERY

TOWARDS TEN YEARS OF MILELE ZANZIBAR FOUNDATION, READ THE ACHIEVEMENTS OF THE SHEHIA PROJECT

MABADILIKO YA HALI YA HEWA NITISHIO LINALOWAKABILI WANAWAKE WAJAWAZITO NA WATOTO.

MTI WA MATUMAINI WA ZINDULIWA ARUSHA: UNICEF

Tanzania Kids Time August 14, 2022
Share this Article
Facebook Twitter Email Print
Previous Article VIJANA WAOMBA SOMO LA STADI ZA MAISHA KUFUNDISHWA SHULENI
Next Article ISSA IBRAHIM MGONJWA WA MWISHO WA POLIO TANZANIA
Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

Facebook Like
Twitter Follow
Youtube Subscribe
Telegram Follow
- Advertisement -
Ad image

Latest News

Mapendekezo ya Mradi wa Sauti zetu ni Muhimu kwa Mkakati wa Elimu Jumuishi
Elimu Haki Za Watoto
Mafanikio ya Shirika la SAWA Kuwezesha Wazazi Kuziishi Stadi za Maisha na Maadili
Elimu
Sababu ya Mradi wa ALiVE Kufanikiwa Kutengeneza Vinara Zaidi ya 300 Tanzania
Elimu Haki Za Watoto
KONGANI YA ELIMU YA MTANDAO WA ELIMU WA KIKANDA – RELI AFRIKA YAONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WALIMU DUNIANI.
Elimu
//

Tanzania Kids Time: A platform spotlighting children’s and women’s issues in Tanzania, focusing on education, health, and environmental conservation.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

© 2023 Tanzania Kids Time. Powered by Digital Media Innovation Program. All Rights Reserved.

Join Us!

Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..

Zero spam, Unsubscribe at any time.

Removed from reading list

Undo
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?