By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
Tanzania Kids Time
  • Home
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Mazingira
  • Uchambuzi na Takwimu
  • Wasiliana Nasi
Reading: ISSA IBRAHIM MGONJWA WA MWISHO WA POLIO TANZANIA
Share
Notification Show More
Latest News
Mapendekezo ya Mradi wa Sauti zetu ni Muhimu kwa Mkakati wa Elimu Jumuishi
Elimu Haki Za Watoto
Mafanikio ya Shirika la SAWA Kuwezesha Wazazi Kuziishi Stadi za Maisha na Maadili
Elimu
Sababu ya Mradi wa ALiVE Kufanikiwa Kutengeneza Vinara Zaidi ya 300 Tanzania
Elimu Haki Za Watoto
KONGANI YA ELIMU YA MTANDAO WA ELIMU WA KIKANDA – RELI AFRIKA YAONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WALIMU DUNIANI.
Elimu
TANZANIA WILL HOST CIGOFA4 TO FIND CONCRETE SOLUTIONS FOR YOUTH LAND QUESTIONS
Editor's Pick
Aa
Aa
Tanzania Kids Time
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Home
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Uchambuzi na Takwimu
  • Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi
  • Contact
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Tanzania Kids Time > Blog > Afya > ISSA IBRAHIM MGONJWA WA MWISHO WA POLIO TANZANIA
AfyaUncategorized

ISSA IBRAHIM MGONJWA WA MWISHO WA POLIO TANZANIA

Tanzania Kids Time
Last updated: 2024/01/29 at 2:30 PM
By Tanzania Kids Time 6 Min Read
Share
SHARE

Polio ni nini:

Kwa mujibu wa Wizara ya Afya nchini Tanzania inatoa ufafanuzi kuhusu mlipuko wa ugonjwa wa polio kuwa ni ugonjwa unaosababishwa na kirusi ambacho huambukizwa kutoka kwa mtu aliyeathirika kwenda kwa mwingine, kwa kula au kunywa kitu kilicho chafuliwa na kinyesi chenye virusi vya polio. Virusi vya polio vinapoingia mwilini huathiri mfumo wa fahamu na kusababisha madhara ya kiafya ikiwa ni pamoja na kupooza kwa ghafla kwa kiungo au viungo na hata kupelekea kifo.

Dalili:
Dalili za awali za ugonjwa wa polio ni pamoja na homa, uchovu, maumivu ya kichwa, kutapika, kukakamaa shingo na maumivu ya viungo, na kundi linalo athirika Zaidi ni watoto walio chini ya umri wa miaka mitano 5.

Chanjo ya polio:
Nizaidi ya miaka arobaini (45) tangu Tanzania ianze zoezi la utoaji chanjo za kuzuia mlipuko wa ugonjwa polio na zoezi la utoaji chanjo ya kwanza ilianza kutolewa mnamo mwaka 1975.

Lini wagonjwa wa mwisho wa polio waligundulika Tanzania?
Kwamujibu wa Dr. Anthony Kazoka kutoka shirika la afya ulimwenguni (WHO) ofisi za Tanzania nilipo fanya nae mahojiano maalumu kuhusu mwenendo wa mlipuko wa ugonjwa wa polio nchini na utoaji chanjo Amesema.

Kwa mara ya mwisho wagonjwa wa polio waligundulika kwenye mikoa mitatu ya Tanzania bara, mgonjwa wa kwanza aligundulika tarehe 11 mwezi Julai mwaka 1996 Mkoani Arusha, Mgonjwa wapili aligundulika tarehe 24 mwezi Julai mwaka 1996 Mkoani Kigoma na mgonjwa wa tatu na wa mwisho aligundulika tarehe 30 mwezi Julai mwaka 1996 Mkoani Mtwara.

Shuhuda wa ugonjwa huu Tanzania ni nani?
Ilikupata uhalisia Zaidi kuhusu changamoto za ugonjwa huu wa polio nimemtafuta mgonjwa wa wamwisho kugundulika na virusi vya polio nchini Tanzania ndugu Issa Ibrahim alie gundulika tarehe 30 mwezi Julai mwaka 1996 Mkoani Mtwara.

“Nilizaliwa Wilaya ya Mtwara vijijini Mkoani Mtwara, wakati nikiwa na umri wa miaka mitatu sikumoja nilienda uani kujisaidia sasa wakati ninarudi ghafla mguu wangu wa kushoto ukaisha nguvu nikadondoka chini, nikajaribu kunyanyuka ikashindikana.

Basi nikapiga kelele za kuhitaji msaada.nikaita mamaaaaa!!!!!!!!!!!!! Mama alikuja alipofika nika mwambia nimeshindwa kutembea akaninyua akajaribu kunisimamisha lakini mguu ukaanza kukakamaa na kuuma sana, akanibeba akanipeleka ndani kunikalisha.

Basi!! Baadae hali ile hikurejea kwenye ukawaida wake baba alipofika mama akamueleza jinsi ilivyo tokea mwanzo hadi mwisho, jambo la kushangaza baba akasema huyu mtoto amelogwa sio ugonjwa wakawaida hakuna haja ya kumpeleka hospitali huko nikupoteza muda na pesa, baba akawa anamwambia mama maneno hayo.

Mama hakunikatia tamaa sasa nimekuwa mtu wa kubebwa wakati wote au wanapo niacha ndipo watakapo nikuta maana siwezi kunyanyua tena mguu na kutembea, siku moja akanipeleka kituo cha afya nilipo pimwa ndio nikagundulika nina polio, ila imeathiri muguu wataalamu wa afya wakamshauri mama niwe nakisaidizi cha mkuu kwamaana ya kutembea na magongo”.

Maendeleo yake yakoje mpaka sasa?
Ninaendelea vizuri maana nilipona polio laikini iliniachia maumivu makali kwenye mguu wangu wakushoto, siwezi kufanya kazi ngumu kwa muda mrefu nikiwa nimesimama kunawakati ukifika unaisha nguvu ahata kama ninatembea inabidi nisitishe safari nikae kwanza ukipoa ndio niendelee na safari.


Ushauri wake kwa jamii ni upi?
Ibrahim anaishauri jamii kulingana na uzoefu alioupata kupitia ugonjwa wa polio tangu mwaka 1996 na kupatiwa matibabu, japokuwa amebakiwa na ulemavu wa kupooza mguu hayo yote nilisimuliwa na mama yangu baada ya kufikia umri wa kujitambua, “anasema wazazi/walezi wasije kuwa kama baba yangu alie kata kunihudumia na kunipeleka hospitali akisema nimelogwa, hakikisheni mnawapeleka watoto kupata chanjo kila wakati unapofika ilikuepuka ulemavu wa kudumu na hata vifo wakati mwingine”.


Issa Ibrahim yupo wapi kwa sasa?
Ibrahim kwa sasa anaishi Dar es Salaam kwa mama yake mdogo, ambapo hivi karibuni Mh.Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amewaagiza watendaji wa Wizara hiyo kumpatia kitengo ndani ya Wizara hiyo Nd.Ibrahim hususani kwenye kitengo cha elimu kwa umma ilikuendelea kuhamasisha chanjo ya polio nchini.

Hali ya mlipuko wa polio kwa sasa ikoje Tanzania?
Hata hivyo Dr. Anthony Kazoka amesema tangu mwaka 1996 hakuna kisa chochote cha mgonjwa wa polio nchini, na hii nikutokana na jitihada za serikali kupitia Wizara ya afya kwa kushirikiana na shirika la afya ulimwenguni (WHO) ofisi za Tanzania kuhakikisha wanadhibiti mlipuko huo kwa kuanzisha kampeini za utoaji chanjo kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano.

Visa vya polio vimepungua kwa zaidi ya 99% tangu 1988, kutoka wastani wa visa 350,000 kwenye zaidi ya nchi 125 zenye ugonjwa huo hadi visa 175 vilivyoripotiwa mnamo mwaka 2019 duniani kote wakati huo Tanzania kukiwa hakuna kisa chochote cha polio tangu mwaka 1996, hatua iliyosababisha- WHO kanda ya afrika kuiweka Tanzania kwenye orodha ya nchi zilizo tokomeza mlipuko huo wa polio na kubakia kwenye nchi za Pakistan na Afghanistan.

Na, John Kabambala
Mwandishi wa habari za watoto Tanzania.
[email protected]

You Might Also Like

ENERGY AND NEO-COLONIALISM IN AFRICA, NO ANSWERS?

THROUGH MZF NOW TRADITIONAL BIRTH ATTENDANCE THEY IMPROVE WOMEN’S WELL-BEING FOR SAFE DELIVERY

TOWARDS TEN YEARS OF MILELE ZANZIBAR FOUNDATION, READ THE ACHIEVEMENTS OF THE SHEHIA PROJECT

MABADILIKO YA HALI YA HEWA NITISHIO LINALOWAKABILI WANAWAKE WAJAWAZITO NA WATOTO.

MTI WA MATUMAINI WA ZINDULIWA ARUSHA: UNICEF

Tanzania Kids Time September 1, 2022
Share this Article
Facebook Twitter Email Print
Previous Article WANAWAKE WANAONYONYESHA WAAHIDI KUZINGATIA MLO WA MAKUNDI MATANO YA VYAKULA
Next Article JINSI YA KUBORESHA MTAALA WA ELIMU YA AWALI
Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

Facebook Like
Twitter Follow
Youtube Subscribe
Telegram Follow
- Advertisement -
Ad image

Latest News

Mapendekezo ya Mradi wa Sauti zetu ni Muhimu kwa Mkakati wa Elimu Jumuishi
Elimu Haki Za Watoto
Mafanikio ya Shirika la SAWA Kuwezesha Wazazi Kuziishi Stadi za Maisha na Maadili
Elimu
Sababu ya Mradi wa ALiVE Kufanikiwa Kutengeneza Vinara Zaidi ya 300 Tanzania
Elimu Haki Za Watoto
KONGANI YA ELIMU YA MTANDAO WA ELIMU WA KIKANDA – RELI AFRIKA YAONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WALIMU DUNIANI.
Elimu
//

Tanzania Kids Time: A platform spotlighting children’s and women’s issues in Tanzania, focusing on education, health, and environmental conservation.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

© 2023 Tanzania Kids Time. Powered by Digital Media Innovation Program. All Rights Reserved.

Join Us!

Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..

Zero spam, Unsubscribe at any time.

Removed from reading list

Undo
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?