By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
Tanzania Kids Time
  • Home
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Mazingira
  • Uchambuzi na Takwimu
  • Wasiliana Nasi
Reading: RIPOTI YA ALiVE YAWASILISHWA KWA WAHARIRI NA WAWAKILISHI WA VYOMBO VYA HABARI
Share
Notification Show More
Latest News
Mapendekezo ya Mradi wa Sauti zetu ni Muhimu kwa Mkakati wa Elimu Jumuishi
Elimu Haki Za Watoto
Mafanikio ya Shirika la SAWA Kuwezesha Wazazi Kuziishi Stadi za Maisha na Maadili
Elimu
Sababu ya Mradi wa ALiVE Kufanikiwa Kutengeneza Vinara Zaidi ya 300 Tanzania
Elimu Haki Za Watoto
KONGANI YA ELIMU YA MTANDAO WA ELIMU WA KIKANDA – RELI AFRIKA YAONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WALIMU DUNIANI.
Elimu
TANZANIA WILL HOST CIGOFA4 TO FIND CONCRETE SOLUTIONS FOR YOUTH LAND QUESTIONS
Editor's Pick
Aa
Aa
Tanzania Kids Time
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Home
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Uchambuzi na Takwimu
  • Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi
  • Contact
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Tanzania Kids Time > Blog > Elimu > RIPOTI YA ALiVE YAWASILISHWA KWA WAHARIRI NA WAWAKILISHI WA VYOMBO VYA HABARI
Elimu

RIPOTI YA ALiVE YAWASILISHWA KWA WAHARIRI NA WAWAKILISHI WA VYOMBO VYA HABARI

Tanzania Kids Time
Last updated: 2024/01/29 at 2:30 PM
By Tanzania Kids Time 8 Min Read
Share
SHARE

Warsha iliyowakutanisha Wahariri na wawakilishi wa vyombo vya Habari nchini Tanzania iliyoandaliwa na Shirikia la Gesci kutoka Nchini Kenya kwa kushirikiana na Taasisi ya Milele Zanzibar Foundation kutoka Zanzibar ilifanyika Jumamosi ya tarehe 11 March 2023 katika Hoteli ya Double View iliyopo Kata ya Sinza Halmashauri ya Wilaya ya Ubungo Jijini Dar es salaam kwa ajili ya kuitamburisha Ripoti ya ALiVE kwa wanahabari, pamoja na kuutamburisha Mradi wa ADAPT.

Samson John Sitta Mratibu wa Mradi wa ALiVE nchini Tanzania katika mahojiano baada ya Warsha, ameiambia Tanzania Kids Time kwamba pamoja na lengo la Warsha hiyo ya Siku moja kuwa ni kuitamburisha Ripoti ya Tathmini ya upimaji Stadi za maisha na maadili kwa vijana (13 – 17) Afrika mashariki (ALiVE), lakini pia ilikua ni kutoa taarifa ya utafiti kutoka katika Mradi mwingine wa ADAPT na kuwaeleza wanahabari namna gani ripoti hizo zitatumika kufanya uchechemuzi katika Sera za Nchi ili kuleta maboresho ya mitaala ya Elimu.

“Lengo la kukutana hapa ilikua ni kuwapitisha wanahabari katika Ripoti yetu ya upimaji wa Stadi za maisha kwa vijana wa umri wa miaka 13 – 17 Afrika mashariki, pamoja na hilo tulikua tunawasilisha taarifa nyingine ya mradi mwingine wa ADAPT ambao ni Mradi Dada wa ALiVE unaohakikisha baada ya utafiti na Ripoti kutoka ni kwa namna gani matokeo yake yanaweza kutumika katika kufanya uchechemuzi katika Sera” Alisema Samson John Sitta, hii hapa ni sauti ya Samson John Sitta.

Uzinduzi wa Ripoti ya ALiVE ulifanyika jijini Dar es salaam mnamo Januari 26, 2023.

 

https://tanzaniakidstime.org/wp-content/uploads/2023/03/RIPOTI-YA-ALiVE-YAWASILISHWA-KWA-WAHARIRI-NA-WAWAKILISHI-WA-VYOMBO-VYA-HABARI.mp3

 

Mwandishi wa Habari Hughes Dugilo kutoka Dar es salaam alikua miongoni mwa wanahabari walioshiriki katika Warsha ya iliyoandaliwa na Shirika la Gesci, alishukuru na kupongeza kwa jinsi miradi hiyo miwili inavyoshirikiana kutoa matokeo ya mahili za Stadi za maisha na maadili kwa vijana wa Afrika ya mashariki na kuhakikisha hatua zinachukuliwa kwa watunga Sera kisha Serikali kuchukua hatua ya kufanya mabadiliko, lakini pia alieleza namna alivyo na wajibu katika kuhabarisha Jamii kuhusu Stadi za maisha na maadili.

Mwandishi wa Habari Hughes Dugilo alisema, “kwanza nipongeze miradi ya ALiVE na ADAPT, leo tumeongeza ufahamu zaidi kuhusu Stadi za Maisha na Maadili, tukizungumzia Stadi za maisha tunagusa maeneo mengi, masuala ya kujitambua, kujitegemea na mimi kama Mwandishi wa Habari nina wajibu mkubwa sana baada ya Warsha hii, kwanza kutekeleza majukumu yangu katika kuihabarisha Jamii kwa ujumla kuhusu Stadi za maisha kwa vijana. Adhima ni kuona vijana wazitambua stadi za maisha, wazisimamie na waziishi ili baadae waje kuwa watu wa kulisaidia Taifa letu” Sauti ya Hughes Dugilo. 

https://tanzaniakidstime.org/wp-content/uploads/2023/03/RIPOTI-YA-ALiVE-YAWASILISHWA-KWA-WAHARIRI-NA-WAWAKILISHI-WA-VYOMBO-VYA-HABARI-2.mp3
JINSI MRADI WA ALiVE ULIVYOTOA RIPOTI BARA NA VISIWANI.

Mradi wa ALiVE ambao uko chini ya Taasisi Milele Zanzibar Foundation, ulifanya tathmini yake ya upimaji Stadi za maisha na maadili kwa vijana Afrika mashariki kwanzia Mwaka wa 2020 hadi 2022 upande wa Zanzibar na Tanzania Bara ili kuangalia Mahili za Stadi za Maisha na Maadili waliyonayo vijana katika Halmashauri za Wilaya 45 (Wilaya 11 kutokaTanzania visiwani na 34 za Tanzania Bara).

Mradi wa upimaji Stadi za Maisha na Maadili kwa vijana wa umri wa miaka 13-17 uliofanywa na Taasisi ya Milele Zanzibar Foundation kutoka Zanzibar ulijikita kutafiti Stadi za Maisha Tatu ambazo ni kujitambua, ushirikiano, utatuzi wa matatizo pamoja na kutafiti Tunu (Maadili) ya Heshima, ambapo upande wa Zanzibar jumla ya vijana wa kike na wakiume 2,447 wamehojiwa katika Kaya 1,942.

Upande wa Tanzania Bara Mradi wa ALiVE umewafikia vijana 14,645 katika Kaya 11,802.

KWA NINI MRADI WA ADAPT KUTOKA SHIRIKA LA GESCI UNAHUSIKA.

Kwa mujibu wa Ramadhani Matimbwa Mratibu wa Mradi wa ADAPT Kutoka Shirika la GESCI la nchini Kenya, Mradi wa ADAPT ambao kirefu chake ni (Adapting of Assesment into Policy and Learning) mradi ambao umejikita kufuatilia hatua kwa hatua namna matokeo ya tafiti yanavyoweza kutumika vyema katika kufanya uchechemuzi kwa watunga Sera na kuleta mabadiliko chanya ya tafiti hizo.

“ADAPT Pia inajaribu kuchechemua tafiti za ALiVE namna tunavyojenga uwezo wetu sisi ni kwa kujadili hizi tafiti mbalimbali, tunawaita watu kwa pamoja tunawaeleza kile tunachokiamini ili kwa pamoja tukielewana mnaweza kujenga jambo Fulani lakini pia tunavyokutana na wahariri na wanahabari kwetu inatusaidia kufikisha taarifa hizi kwa Jamii na Serikali kwa sababu ADAPT lengio lake kubwa ni kufanya mabadiliko, sasa mabadiliko yale huwa yaanzia kwenye mijadala” Alisema Ramadhani Matimbwa, na hii hapa ni sauti yake. 

https://tanzaniakidstime.org/wp-content/uploads/2023/03/RIPOTI-YA-ALiVE-YAWASILISHWA-KWA-WAHARIRI-NA-WAWAKILISHI-WA-VYOMBO-VYA-HABARI-3.mp3
Soma zaidi kuhusu GESCI inayotekeleza Mradi wa ADAPT: Home – The Global e-Schools and Communities Initiative (GESCI)

MFANO WA YALIYOMO KATIKA RIPOTI YA ALiVE TANZANIA VISIWANI.

Kutoka katika ukurasa wa Tano wa Ripoti ya ALiVE Zanzibar kipengele cha Stadi ya Maisha ya “UTATUZI WA MATATIZO” Ripoti imebainisha 23% ya vijana wanapata wakati mgumu kutambua tatizo au asili yake kimtazamo na kwa hivyo hawawezi kutambua suluhisho lake.

Asilimia 48% ya vijana wanauwezo wa kutambua uwepo wa tatizo kutoka kwa mtu kimtazamo na kuchukua hatua ili kutambua uwezekano wa kupata suluhisho, 15% ya vijana wanauwezo wa kutambua uwepo wa tatizo kutoka kwa mtu kimtazamo, kutambua njia kuu za kutatua tatizo na kuweza kusuluhisha.

Lakini pia Ripoti imesema 14% ya vijana wanauwezo wa kutambua uwepo wa tatizo kutoka kwenye mitazamo mingi, kuwa na njia nyingi za suluhisho na kuchagua njia ipi inaweza kutumika kutatau tatizo.

SHIRIKA LA RELI LILIVYOFANIKISHA KUPATIKANA KWA MIRADI YA ALiVE NA ADAPT

Mtandao wa Elimu Afrika Mashariki unaofahamika kwa jina la RELI, (Regional Education Learning Initiative in East Africa) unafanya kazi katika Nchi Tatu za Afrika ya Mashariki ambazo ni Kenya, Uganda na Tanzania ambao hadi sasa una zaidi ya wanachama 70 ambao ni mashirika mbalimbali yasiyo ya kiserikali kwa lengo la kuhakikisha ujifunzaji jumuishi kwa watoto wote katika Afrika Mashariki.

Mradi wa ALiVE unaotekelezwa na Taasisi ya Milele Zanzibar Foundation umetoka katika Kongani ya Stadi za Maisha na maadili ikiwa ni moja ya Kongani Nne zilizopo katika Mtandao wa RELI.

Mradi wa ADAPT unaotekelezwa na Shirika la Gesci kutoka nchini Kenya nao pia unatoka katika Kongani ya Stadi za Maisha na Maadili kwa lengo la kuleta mabadiliko kupitia ufuatiliaji wa matokeo ya tafiti mbalimbali na kuona kwa namna gani watunga sera wanaweza kuleta mabadiliko.

Ifahamu kwa undani RELI: RELI – Regional Education Learning Initiative in East Africa (reliafrica.org)

You Might Also Like

Mapendekezo ya Mradi wa Sauti zetu ni Muhimu kwa Mkakati wa Elimu Jumuishi

Mafanikio ya Shirika la SAWA Kuwezesha Wazazi Kuziishi Stadi za Maisha na Maadili

Sababu ya Mradi wa ALiVE Kufanikiwa Kutengeneza Vinara Zaidi ya 300 Tanzania

KONGANI YA ELIMU YA MTANDAO WA ELIMU WA KIKANDA – RELI AFRIKA YAONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WALIMU DUNIANI.

UWEZO TANZANIA YARATIBU KIKAO CHA MIKAKATI YA KUWASHIRIKISHA WAZAZI UELIMISHAJI VIJANA STADI ZA MAISHA.

Tanzania Kids Time March 13, 2023
Share this Article
Facebook Twitter Email Print
Previous Article SIKU YA WANAWAKE DUNIANI NI SULUHU KWA WATOTO WAKIKE
Next Article RIPOTI YA ALiVE YAWASILISHWA KWA WAHARIRI NA WAWAKILISHI WA VYOMBO VYA HABARI
Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

Facebook Like
Twitter Follow
Youtube Subscribe
Telegram Follow
- Advertisement -
Ad image

Latest News

Mapendekezo ya Mradi wa Sauti zetu ni Muhimu kwa Mkakati wa Elimu Jumuishi
Elimu Haki Za Watoto
Mafanikio ya Shirika la SAWA Kuwezesha Wazazi Kuziishi Stadi za Maisha na Maadili
Elimu
Sababu ya Mradi wa ALiVE Kufanikiwa Kutengeneza Vinara Zaidi ya 300 Tanzania
Elimu Haki Za Watoto
KONGANI YA ELIMU YA MTANDAO WA ELIMU WA KIKANDA – RELI AFRIKA YAONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WALIMU DUNIANI.
Elimu
//

Tanzania Kids Time: A platform spotlighting children’s and women’s issues in Tanzania, focusing on education, health, and environmental conservation.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

© 2023 Tanzania Kids Time. Powered by Digital Media Innovation Program. All Rights Reserved.

Join Us!

Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..

Zero spam, Unsubscribe at any time.

Removed from reading list

Undo
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?