By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
Tanzania Kids Time
  • Home
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Mazingira
  • Uchambuzi na Takwimu
  • Wasiliana Nasi
Reading: TMDA INAVYO SHUGHULIKIA AFYA ZA WATOTO:
Share
Notification Show More
Latest News
Mapendekezo ya Mradi wa Sauti zetu ni Muhimu kwa Mkakati wa Elimu Jumuishi
Elimu Haki Za Watoto
Mafanikio ya Shirika la SAWA Kuwezesha Wazazi Kuziishi Stadi za Maisha na Maadili
Elimu
Sababu ya Mradi wa ALiVE Kufanikiwa Kutengeneza Vinara Zaidi ya 300 Tanzania
Elimu Haki Za Watoto
KONGANI YA ELIMU YA MTANDAO WA ELIMU WA KIKANDA – RELI AFRIKA YAONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WALIMU DUNIANI.
Elimu
TANZANIA WILL HOST CIGOFA4 TO FIND CONCRETE SOLUTIONS FOR YOUTH LAND QUESTIONS
Editor's Pick
Aa
Aa
Tanzania Kids Time
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Home
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Uchambuzi na Takwimu
  • Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi
  • Contact
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Tanzania Kids Time > Blog > Afya > TMDA INAVYO SHUGHULIKIA AFYA ZA WATOTO:
Afya

TMDA INAVYO SHUGHULIKIA AFYA ZA WATOTO:

Tanzania Kids Time
Last updated: 2024/01/29 at 2:30 PM
By Tanzania Kids Time 7 Min Read
Share
SHARE

 

UTANGULIZI:

Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba
(TMDA) ni Taasisi ya Serikali iliyo chini ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto yenye jukumu la kudhibiti ubora, usalama na
ufanisi wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi.

 UMUHIMU WA AFYA YA WATOTO:

Taifa
linapaswa kulindwa na miongoni mwa vitumuhimu ni matumizi ya madawa na vifaa
tiba na vitendanishi vinavyo tumika kwa watoto, watoto watakapo pewa  au kutumia bidhaa hii ya dawa pasipo
kuthibitishwa na mamlaka husika matokeo yake kizazi hicho kunahatari ya
kuteketea, hivyo basi ndiomaana, mwaka 2018, TMDA ilifanya ukaguzi wa viwanda
vya kusindika vyakula vya nyongeza na maziwa ya watoto wachanga vilivyopo nje
ya nchi ili kujilidhisha kabla ya kuruhusiwa kuingiza sokoni.  

MAJUKUMU  YA TMDA KATIKA
KULINDA AFYA ZA WATOTO:

TMDA hupokea maombi ya usajili wa
vifaa tiba nchini vikiwemo vinavyotumika kwa watoto kutoka kwa wadau mbalimbali
walioko ndani na nje ya nchi, Baada ya kupokea maombi hufanya tathmini ya
taarifa za ubora, usalama na ufanisi wa Vifaa tiba vilivyowasilishwa na pale
inaporidhika na tathmini husika ya vifaa hivyo husajiliwa.

 Upimaji
wa sampuli katika maabara.

Maabara ya TMDA hupima sampuli za
vifaa tiba kwa lengo la kuhakiki ubora, usalama na ufanisi wake kabla na
baada ya kuruhusiwa kuingia katika soko, Pale inapobainika kwamba kifaa tiba
hakikidhi viwango vya usalama, ubora na ufanisi hakipewi usajili na kama kipo
sokoni matumizi yake husitishwa na kuondolewa.

 Kudhibiti
uingizaji na usafirishaji nje ya nchi.

TMDA hudhibiti uingizaji nchini
wa vifaa tiba na Dawa kwa
kuwataka waagizaji kuomba kibali cha kuingiza
vifaa tiba nchini na kufanya ukaguzi kwenye vituo vya forodha
kuhakiki kama waagizaji wamezingatia
taratibu za uingizaji vifaa tiba.

 Ukaguzi
katika soko na vituo vya forodha.

TMDA hufanya ukaguzi katika vituo
vya forodha, maeneo ya biashara ikiwa ni pamoja na maduka, maghala na vituo vya
kutolea huduma za afya kwa nia ya kuhakiki usalama, ubora na ufanisi wa vifaa
tiba na Dawa, Pale inapobainika kwamba kuna ukiukwaji wa sheria, kanuni na
taratibu, Mamlaka huchukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutoa onyo,
kusitisha kwa muda matumizi ya kifaa tiba hadi marekebisho yafanyike au kufuta
usajili wa kifaa tiba kufikisha mtuhumiwa mahakamani pale inapolazimu.

 FAMASI ZINAFANYA NINI KULINDA AFYA ZA WATOTO.

Maeneo ambayo huleta changamoto
kubwa kwa jamii ni maduka
  ya dawa
muhimu, baadhi yao huuza dawa na vifaa tiba vilivyo isha muda wake kwa baadhi
yao, kwa nini hutokea hali hii? Je, ni njiagani hutumika kuhifadhi dawa na
vifaa tiba kwenye maduka ya dawa? Nimetembelea moja kati ya maduka ya kuuza dawa
muhimu Marhaba farmasi iliopo Mkoani Morogoro, na nimefanya mahojiano na
Kelvin Magonda huyu ni mfamasia
sikiliza mahojiano hayo….
https://appfasta.com/tkt/cms/ 

 Mafanikio ya TMDA katika Kulinda Afya za Watoto

CHANGAMOTO ZINAZOIKABILI TMDA KULINDA AFYA ZA WATOTO

Mkuu wa Mawasiliano kutoka TMDA Bi, Gaudensia Simwanza
amebainisha  changamoto mojawapo kwa
jamii ni ununuzi holela na kutumia dawa bila kufanyiwa uchunguzi au kuelekezwa
na daktari, kutumia vijiuasumu kutibu magonjwa yanayotokana na virusi (viral
infections) kutumia dozi isiyosahihi au kushindwa kumaliza dozi, kutumia dawa
zinazoingiliana
kiutendaji kwa pamoja, kwa mfano tetracycline
na Magnesium kutumia dawa na pombe. Jambo linguine
kubwa ununuzi wa dawa au kifaa tiba kilicho maliza muda wake wa matumizi, na
kushindwa kutoa taarifa kwa mamlaka husika kama vile TMDA.

ELIMU GANI HUTOLEWA NA TMDA KWA JAMII?

Elimu inayo tolewa na TMDA ni kuhusu
matumizi sahihi ya bidhaa kupitia shule za sekondari na msingi, makundi
mbalimbali ya wananchi na vikundi vya wajasiriamali, Lengo la elimu hiyo ni
kuimarisha udhibiti wa sekta hiyo ili kuhakilisha kuwa huduma za usambazaji na
uuzaji wa dawa, vifaa tiba  na
vitendanishi inatolewa bila kuathiri usalama wa chakula na kusababisha madhara
ya kiafya kwa walaji.

 Elimu kwa umma husaidia kuongeza
uelewa kwawatumiaji wa bidhaa zinazodhibitiwa na TMDA na
wananchi kwa
ujumla katika matumizi sahihi ya
bidhaa na kuongeza utii wa Sheria bila
shuruti.

 DHIMA ya TMDA  ni Kulinda afya ya jamii kwa kuzuia
athari zinazoweza kujitokeza kutokana na matumizi ya dawa, vifaa tiba na vitendanishi.

 DIRA ya TMDA ni  Kuwa Mamlaka inayoongoza katika kudhibiti
ubora, usalama, na ufanisi wa dawa, Vifaa tiba, vitendanishi na bidhaa nyingine
za afya kwa wote.

 FALSAFA ya TMDA ni Kutoa huduma
bora za udhibiti katika kulinda afya ya jamii na mazingira kwa kutumia
wafanyakazi wenye ujuzi na ari ya kazi.

 USHAURI

Ili kuepuka au kupunguza kutokea
usugu wa bakteria unashauriwa kutumia dawa kwa usahihi, Usinunue vijiuasumu
kiholela, Usinunue vijiuasumu bila cheti cha Daktari, Hakikisha unafahamu
matumizi sahihi ya dawa ulizopewa kabla ya kurudi nyumbani toka kituo cha afya
au duka la dawa na
 Tumia dozi sahihi kwa kipindi.

 TMDA inawataka watengenezaji,
waagizaji na wauzaji wa vifaa tiba kufuata taratibu na kujihakikishia ubora,
usalama na ufanisi wa vifaa tiba wanavyonuia kuviuza kwenye soko la Tanzania
kabla ya kukaguliwa na kuhakikiwa na Mamlaka, hii itarahisisha udhibiti wa
vifaa tiba nchini na kuongeza imani ya watumiaji na wananchi kwa bidhaa
zinazouzwa.

 Vile vile, jamii inaombwa kutoa
taarifa TMDA au kituo chochote cha afya inapobaini ukiukwaji wa taratibu za
utengenezaji, usambazaji, uuzaji na matumizi yasiyo sahihi ya vifaa tiba ili
mwisho wa yote lengo la Serikali la kulinda afya ya wananchi wakiwemo watoto liwezekutimia.

Na, John Kabambala-Morogoro.

You Might Also Like

THROUGH MZF NOW TRADITIONAL BIRTH ATTENDANCE THEY IMPROVE WOMEN’S WELL-BEING FOR SAFE DELIVERY

TOWARDS TEN YEARS OF MILELE ZANZIBAR FOUNDATION, READ THE ACHIEVEMENTS OF THE SHEHIA PROJECT

MABADILIKO YA HALI YA HEWA NITISHIO LINALOWAKABILI WANAWAKE WAJAWAZITO NA WATOTO.

MTI WA MATUMAINI WA ZINDULIWA ARUSHA: UNICEF

LISHE BORA NI MTAJI: NIMUHIMU KUWEKEZA KWA WATOTO,FAO:

Tanzania Kids Time April 21, 2023
Share this Article
Facebook Twitter Email Print
Previous Article FAHAMU HALI YA UKATILI KWA WATOTO MKOA WA MOROGORO:
Next Article JUMA LA ELIMU 2023: TENMET INAHAMASISHA UCHANGIAJI WA UBORESHAJI ELIMU
Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

Facebook Like
Twitter Follow
Youtube Subscribe
Telegram Follow
- Advertisement -
Ad image

Latest News

Mapendekezo ya Mradi wa Sauti zetu ni Muhimu kwa Mkakati wa Elimu Jumuishi
Elimu Haki Za Watoto
Mafanikio ya Shirika la SAWA Kuwezesha Wazazi Kuziishi Stadi za Maisha na Maadili
Elimu
Sababu ya Mradi wa ALiVE Kufanikiwa Kutengeneza Vinara Zaidi ya 300 Tanzania
Elimu Haki Za Watoto
KONGANI YA ELIMU YA MTANDAO WA ELIMU WA KIKANDA – RELI AFRIKA YAONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WALIMU DUNIANI.
Elimu
//

Tanzania Kids Time: A platform spotlighting children’s and women’s issues in Tanzania, focusing on education, health, and environmental conservation.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

© 2023 Tanzania Kids Time. Powered by Digital Media Innovation Program. All Rights Reserved.

Join Us!

Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..

Zero spam, Unsubscribe at any time.

Removed from reading list

Undo
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?