By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
Tanzania Kids Time
  • Home
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Mazingira
  • Uchambuzi na Takwimu
  • Wasiliana Nasi
Reading: MAHAKAMA YAWAFIKIA WANANCHI ZAIDI YA 30,000 KUWAPA ELIMU YA SHERIA NDANI YA SIKU 7, MOROGORO
Share
Notification Show More
Latest News
Mapendekezo ya Mradi wa Sauti zetu ni Muhimu kwa Mkakati wa Elimu Jumuishi
Elimu Haki Za Watoto
Mafanikio ya Shirika la SAWA Kuwezesha Wazazi Kuziishi Stadi za Maisha na Maadili
Elimu
Sababu ya Mradi wa ALiVE Kufanikiwa Kutengeneza Vinara Zaidi ya 300 Tanzania
Elimu Haki Za Watoto
KONGANI YA ELIMU YA MTANDAO WA ELIMU WA KIKANDA – RELI AFRIKA YAONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WALIMU DUNIANI.
Elimu
TANZANIA WILL HOST CIGOFA4 TO FIND CONCRETE SOLUTIONS FOR YOUTH LAND QUESTIONS
Editor's Pick
Aa
Aa
Tanzania Kids Time
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Home
  • Afya
  • Elimu
  • Haki Za Watoto
  • Uchambuzi na Takwimu
  • Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi
  • Contact
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Tanzania Kids Time > Blog > Elimu > MAHAKAMA YAWAFIKIA WANANCHI ZAIDI YA 30,000 KUWAPA ELIMU YA SHERIA NDANI YA SIKU 7, MOROGORO
ElimuUchambuzi na Takwimu

MAHAKAMA YAWAFIKIA WANANCHI ZAIDI YA 30,000 KUWAPA ELIMU YA SHERIA NDANI YA SIKU 7, MOROGORO

Tanzania Kids Time
Last updated: 2024/01/29 at 2:30 PM
By Tanzania Kids Time 4 Min Read
Share
SHARE

 

Mahakama kuu Kanda ya
Morogoro imewafikiwa wananchi zaidi ya Elfu Therathini kuwapatia Elimu na
ushauri wa kisheria sambamba na kujibu changamoto zao mbalimbali za kisheria
ndani ya siku saba za maadhimisho ya wiki ya Sheria.

Mafanikio hayo ya
Mahakama yalielezwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama kuu Kanda ya Morogoro, Paul
Joel Ngwembe Februari 02, 2022, katika maadhimisho ya Siku ya Sheria yaliyofanyika
katika viwanja vya Kituo cha haki jumuishi Kihonda, wakati akieleza kazi
zilizofanywa na Mahakama katika kipindi cha Wiki ya Sheria akitaja maeneo
waliyofika na kutoa Elimu, na kwamba wananchi watambue juhudi za hizo ni kwa
ajili yao, kwasababu katika maisha ya Binadamu Sheria haikwepeki.

Jaji Ngwembe pia alizungumzia
maendeleo ya Teknolojia namna ilivyo na kasi, ikileta manufaa makubwa pamoja na
athari ikiwemo Ugonjwa wa Uviko 19, akisema kuwa wamejipanga kuipeleka mahakama
mtandaoni ili kupunguza baadhi ya changamoto zinzoazoweza kujitokeza ikiwemo
Rushwa.

“Mahakama inaamini maisha yote ya
Binadamu yanaongozwa na Sheria, hivyo binadamu hawezi kuikwepa Sheria katika
maisha yake yote” alisema Jaji Mfawidhi Paul Ngwembe.

 “katika maadhimisho haya Wiki ya Sheria Kituo
chetu cha haki jumuishi, tulikua na maeneo tofauti tofauti ya utoaji Elimu,
tulikua na Kituo pale viwanja vya Chamwino, pale Kituo cha mabasi Msamvu,
Kiwanja cha Ndege pale Fire, Soko kuu la Chief Kingalu, tumetembelea Shule za
Msingi Saba, Sekondari Nne, Chuo cha ualimu Kigurunyembe na magereza yote
mawili ambapo ni Gereza la Mahabusu na Gereza la mtego wa Simba’’ aliongeza
Jaji Ngwembe

Serikali ya Mkoa wa
Morogoro ilitoa ahadi ya kuendelea kuwezesha miundombinu ya mawasiliano katika
Mkoa wa Morogoro ili kufanikiwa kwa Mahakama ya kidijitali, alitoa ahadi hiyo Mkuu
wa Wilaya ya Morogoro ALBERTH MSANDO aliyemuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

“Nichukue fursa hii kuahidi kwamba
tutahakikisha tunashirikiana na Mahakama kufikia malengo yake, tunapozungumzia Mahakama
ya kidijitali haiwezi kufanikiwa kama hatutaweka Miundombinu ya mawasiliano
katika maeneo yote, Serikali imeendelea kuwa na mpango wa kuhakikisha kwamba
katika vijiji vyote kunakua na mawasiliano ya Internet (mtandao) kutoka kwenye
vyombo vyetu vya mawasiliano”
alisema
Mkuu wa Wilaya Wakili Msomi, Alberth Msando.

MARIAMU KAPAMA ni
Mwenyekiti msaidizi wa Chama cha wanasheria wa kujitegemea TLS Mkoa wa
Morogoro, alisoma Hotuba yao ambapo Pamoja na mambo mengine alieleza athari za
UVIKO 19 ilivyoathiri utendaji kazi na kuleta madhara kwa baadhi ya wapendwa
wao, akiishauri Mahakama kuitumia Teknolojia vema katika kukabiliana na janga
hilo.

Hotuba ya Ofisi ya
Mwanasheria mkuu wa Serikali, ilisomwa na Wakili Mfawidhi Mkoa wa Morogoro
XAVIER NDALAHWA, Akiahidi Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali itaendelea
kuboresha mfumo wa TEHAMA ili kuunga mkono jitihada za Mahakama.

“Niseme tu kwamba, tumeshuhudia
matumizi ya Mtandao, kusajili na kusikiliza mashauri yakifanikisha katika
utoaji wa Haki hasa katika kipindi cha Uviko 19, ambapo mashauri yalisikilizwa
bila msongamano Mahakamani, mfumo wa mahakama umelea faida kubwa ikiwa ni
pamoja na kuokoa muda na gharama” alisema Xavier Ndalahwa.

Maudhui mengine na jumbe
za Siku ya Sheria nchini yamepambizwa na burudani mbalimbali kutoka kwa
wanamuziki na wanasanaa, CHEDY ELLY SENZIGE ni mtunzi kutoka Morogoro alisoma
Shairi maalumu la Siku ya Sheria.

 ‘’zama za mapinduzi ya nne ya viwanda, safari
ya maboresho kuelekea mahakama mtandaoni’’ ndio kaulimbiu ya Siku ya Sheria
itakayodumu kwa Mwaka wote wa 2022.

Na Hamad Rashid- Morogoro.

You Might Also Like

Mapendekezo ya Mradi wa Sauti zetu ni Muhimu kwa Mkakati wa Elimu Jumuishi

Mafanikio ya Shirika la SAWA Kuwezesha Wazazi Kuziishi Stadi za Maisha na Maadili

Sababu ya Mradi wa ALiVE Kufanikiwa Kutengeneza Vinara Zaidi ya 300 Tanzania

KONGANI YA ELIMU YA MTANDAO WA ELIMU WA KIKANDA – RELI AFRIKA YAONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WALIMU DUNIANI.

UWEZO TANZANIA YARATIBU KIKAO CHA MIKAKATI YA KUWASHIRIKISHA WAZAZI UELIMISHAJI VIJANA STADI ZA MAISHA.

Tanzania Kids Time February 3, 2022
Share this Article
Facebook Twitter Email Print
Previous Article JAMII IMEKUMBUSHWA KUWAJALI WANAWAKE WAJANE NA KUWAPA MSAADA WANAPOHITAJI
Next Article MIMBA ZA UTOTONI ZIMEONGEZEKA MKOA WA MOROGORO KUTOKA 800 HADI ZAIDI YA 1200
Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

Facebook Like
Twitter Follow
Youtube Subscribe
Telegram Follow
- Advertisement -
Ad image

Latest News

Mapendekezo ya Mradi wa Sauti zetu ni Muhimu kwa Mkakati wa Elimu Jumuishi
Elimu Haki Za Watoto
Mafanikio ya Shirika la SAWA Kuwezesha Wazazi Kuziishi Stadi za Maisha na Maadili
Elimu
Sababu ya Mradi wa ALiVE Kufanikiwa Kutengeneza Vinara Zaidi ya 300 Tanzania
Elimu Haki Za Watoto
KONGANI YA ELIMU YA MTANDAO WA ELIMU WA KIKANDA – RELI AFRIKA YAONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WALIMU DUNIANI.
Elimu
//

Tanzania Kids Time: A platform spotlighting children’s and women’s issues in Tanzania, focusing on education, health, and environmental conservation.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

© 2023 Tanzania Kids Time. Powered by Digital Media Innovation Program. All Rights Reserved.

Join Us!

Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..

Zero spam, Unsubscribe at any time.

Removed from reading list

Undo
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?